NEWS

Wednesday 1 April 2020

Watatu wafariki mto Mara


Watu watatu wakiwemo wanawake wajawazito wawili wamekufa maji ndani ya Mto Mara walipokuwa wanavuka kutoka kijiji cha Borenga Wilayani Serengeti kwa mtumbwi wakielekea Nyamongo Wilayani Tarime.
“ Hili tukio lilitokea juzi asubushi na  mtumbwi huo ulikuwa na watu saba na wanne wameokolewa  lakini watatu wamefariki dunia”, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu aliiambia Mara Online News kwa njia ya simu  leo asubuhi
Mkuu huyo wa Wilaya amepiga marufuku matumizi ya mitumbwi katika maeneo jirani yaliyo na mto Mara kutokana na mto huo na mito mingine kujaa maji hivi sasa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages