NEWS

Monday 18 May 2020

Mwenyekiti Halmashauri apania kumng’oa Heche Tarime Vijijini

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Moses Matiko Misiwa, ametangaza rasmi nia yake ya kuvuta fomu ya kuomba kuteuliwa na Chadema kugombea ubunge katika jimbo la Tarime Vijijini mwaka huu.

Misiwa ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nyamwaga, bila shaka atachuana na mbunge wa jimbo hilo anayemaliza muda wake, John Heche, miongoni mwa makada wengine wa chama hicho watakaojitokeza kuomba nafasi hiyo.

Katika mazungumzo yake na Mara Online News hivi karibuni, Misiwa amesema anaamini kwamba kitakachombeba katika kinyang’anyiro hicho ni maendeleo ya Halmashauri ya Wilaya yaliyopatikana chini ya uongozi wake kama mwenyekiti.
Misiwa akizungumza katika moja ya mikutano wa ziara ya viongozi na wananchi

Elimu ilivyopaishwa

Misiwa amesema elimu ni miongoni mwa sekta zilizopata mafanikio makubwa katika kipindi cha uongozi wake kama mwenyekiti wa halmashauri hiyo.

“Tuanze na elimu ya msingi, kwa mara ya kwanza halmashauri yetu imeanzisha shule mpya zaidi ya shule 10. Haya ni mfanikio makubwa katika kuhakikisha watoto wetu wanapata elimu ambayo ni ufunguo wa maendeleo katika jamii yoyote,” amesema.

Misiwa emetaja baadhi ya shule hizo kuwa ni Maika, Nyamiri na Makerero.

Kwa mujibu wa Misiwa, halmashauri hiyo imetumia Sh zaidi ya milioni 700 kutengeneza madawati 1,200 kwa ajili ya wanafunzi wa shule za msingi, hivyo kufanya tatizo lililokuwepo kubaki historia.

“Kwa sasa hakuna mwanafunzi anayekaa chini kwa kukosa dawati katika halmashauri yetu na tumefanikiwa haya yote kwa kutumia mapato ya ndani,” amefafanua Misiwa.

Ameongeza kuwa halmashauri pia imetumia Sh bilioni 1.4 kugharimia ukamilishaji vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari 150.

Kwa upande wa elimu ya sekondari, amesema halmashauri imeweza kujenga shule mpya za sekondari tano; ambazo ni Muriba, Ganyange, Nyansisine na Kewamamba. Katika kata ya Kiore zimejengwa shule mbili.

“Shule hizi mpya zimepokea shilingi zaidi ya milioni 200,” amesema.

Afya yamwagiwa mamilioni

Kwa upande wa sekta ya afya, Misiwa amejivunia ujenzi hospitali mpya ya halmashauri iliyopo Nyamwaga yalipo makao makuu ya halmashuri hiyo.

“Wote ni mashahidi kuwa ilianza kama zahanati na sasa ni hospitali ya halmashauri ya wilaya na tulipitisha shilingi milioni 300 kwa ajili ujenzi na ununuzi wa vifaa, jambo ambalo lilisaidia kuifanya hospitali hiyo kupata usajii na inatoa huduma kwa wananchi wetu,” amefafanua.

Misiwa ametumia nafasi hiyo pia kuwashukuru viongozi wa serikali ambao wamekuwa wakishirikiana kwa karibu katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo wa hospitali.

Aidha, amesema halmashauri hiyo imeweza kuboresha upatikanaji wa huduma katika vituo vya afya.
Wananchi wakipata huduma katika Hosptali mpya ya Tarime DC 
Ametaja vituo hivyo na kiasi cha fedha zilizotolewa na halmashauri kugharimia uboreshaji huduma za afya kwa wananchi kuwa ni  Muriba (Sh milioni 15), Nyanungu (Sh milioni 50), Kerende (Sh milioni 600) kutoka halmashauri na mgodi wa North Mara) na Magoto (Sh milioni 80)

Vituo vingine vya afya ni Sirari (Sh milioni 600) kutoka Serikali Kuu na halmashauri, Kiongera (Sh milioni 80), Mtana (Sh milioni 80) na Nyarwana (Sh milioni 200).

“Upande wa zahanati ni nyingi, lakini nitaje tu Ganyange, Kimusi na Itiryo ambapo tumepeleka shilingi milioni 320,” amesema mwenyekiti huyo wa halmashauri.

Barabara zilivyoboreshwa

Misiwa amesema uwekezaji mkubwa ulielekezwa pia katika kuboresha miundombinu ya barabara ambapo nyingi zilizokuwa hazipitiki sasa zinapitika.
Misiwa akihakikisha kuwa ujenzi wa barabara unaenda sawa 
Amesema Sh zaidi ya bilioni 1.8 zimetumika kuboresha miundombinu ya barabara kupitia Wakala wa Barara Mijini na Vijijini (TARURA).

“Mfano tumezibua njia mpya nyingi kuanzia Nyamwaga – Magoto au Misiwa road, Bikonge - Custom, Mangucha - Nyandage, Taisi - Matamankwe na Bumera – Susuni,” amesema Misiwa na kuongeza:

“Tumetumia mapato ya ndani kuboresha barabara Nyamwaga – Nyanungu yenye urefu wa kilomita 1.5 kwa kiwango cha lami. Pia tumejenga barabara ya Nyamwaga Escarpment – Nyamogo kupitia Kasco kwa kiwango cha lami, hizi zote hazikuwepo.”

Misiwa anaamini wananchi hawatamwangusha katika kinyang’anyiro cha ubunge Tarime Vijijini, hasa ikizingatiwa kuwa usimamizi wake thabiti kama mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ndio umefanikisha miradi hiyo na mingine mingi kwa manufaa ya umma.



Mikopo kwa vijana, wanawake


Misiwa anasema halmashauri hiyo katika mwaka 2014/2015 ilielekeza mkopo wa Sh milioni 36 kwa vikundi vya vijana na wanawake.

“Kwa mara ya kwanza mwaka 2015/2016 nimehakikisha shilingi zaidi ya bilioni 1.2 zinatolewa kwenda kwa vikundi vya vijana na wanawake”, anaongeza Misiwa.

Hati safi halmashauri

Kwa upande mwingine, Misiwa anasema katika kipindi cha uongozi wake, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime imeendelea kupata hati safi kutoka kwa Mthibidi na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG).
Misiwa akionesha hati safi 
“Tangu nimengia hamashauri kwa weledi wangu na uelewa mkubwa kupitia elimu yangu ya sheria na sheria za kimataifa, nimehakikisha halmashauri inapata hati safi miaka yote na sina deni kwa ngazi ya halmashauri na udiwani,” anasema.

Kwanini anataka ubunge?

Misiwa anasema akipata nafasi ya ubunge atawaletea wananchi wa Tarime Vijijini maendeleo makubwa zaidi ya aliyowezesha akiwa mwenyekiti wa halmashauri na diwani.
Misiwa(kulia) kulia akiongoza kikao cha baraza la madiwani 
“Nikipata nafsi ya juu nitafanya zaidi ya niliyofanya nikiwa diwani na mwenyekiti wa halmashauri, maana nitakuwa na wigo mpana kitaifa na kimataifa kupitia diplomatic immunity ya ubunge na nitaendelea kuiungangisha Tarime Vijijini na Serikalai,” anahitimish

(Habari, picha na Mara Online news)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages