NEWS

Monday 5 October 2020

Lilanga aahidi kumaliza changamoto Bariadi

Mgombea ubunge jimbo la Bariadi kwa tiketi ya NCCR Mageuzi, Erasmus Ndege Lilanga

 

MGOMBEA ubunge jimbo la Bariadi kwa tiketi ya NCCR Mageuzi, Erasmus Ndege Lilanga ambaye ni Makamu Askofu wa Kanisa la Spritural Church of Pentecost of Tanzania Kanda ya Mashariki mwa Ziwa ikiwemo mikoa ya Simiyu na Shinyanga, amesema akichaguliwa atakuwa mwepesi wa kutatua changamoto zote kwa wakati.

Lilanga amezitaja baadhi ya kero hizo kuwa ni pamoja na tembo kuvamia mashamba na makazi ya watu ambapo amesema akifanikiwa kuchaguliwa ataweka msukumo serikalini ili litatuliwe haraka.

"Ndugu yangu mwana Bariadi, mimi na wewe tumejionea kwa macho tembo wanavyovamia mashamba na makazi yetu na kuyaharibu kabisa, hivyo nawashauri tena na tena nipeni ridhaa yenu mnichague niwawakilishe katika kuwatetea na kuitaarifu serikali yetu kwa njia mbalimbali bungeni na hata kwa maandishi ikibidi,” amesema jana mara baada ya uzinduzi wa kampeni zake kwenye eneo la stendi ya zamani ya mabasi iliyopo mjini Bariadi, Simiyu.

Erasmus Ndege Lilanga


Mbali na hilo, Lilanga amesema endapo atachaguliwa atahakikisha anakutana na maafisa kilimo wilayani hapa kuona namna bora ya kuboresha kilimo ambacho kitamkwamua mkulima kwa kulima mazao yanayouzika (yenye soko) na hivyo kupata tija kwenye kilimo.

Mgombea huyo ametaja vipaumbele vyake vitano kuwa ni imani juu ya uwepo wa Mungu itawale, amani ya Mungu itawale, ukweli wa Mungu utawale, umoja wa Mungu utawale na agizo la Mungu kila mtu afanyekazi litawale.

Aidha, Lilanga ameahidi kuendelea na kampeni kwa kunadi sera za chama chake na vipaumbele vyake huku akitaja kaulimbiu ya chama hicho kuwa ni "NCCR Mageuzi, utu, itikadi yetu".

(Imeandikwa na Anita Balingilaki, Bariadi)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages