NEWS

Monday 8 February 2021

Mbunge Chege ahimiza ubunifu vyanzo vya mapato Rorya

Mbunge wa Jimbo la Rorya mkoani Mara, Jafari Wambura Chege (kushoto) akishiriki kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya mjini Utegi, leo Februari 8, 2021. Wa tatu kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Ng'ong'a Gerald, Makamu wake, Hores Simba (wa pili kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Charles Chacha (aliyesimama).

MBUNGE wa Jimbo la Rorya mkoani Mara, Jafari Wambura Chege, leo Februari 8, 3021 ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri na kuwataka madiwani kuishauri halmashauri hiyo kubuni vyanzo vya mapato vilivyo imara kwa ajili ya kumudu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wanandi.

 

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Charles Chacha, kikao hicho ni cha bajeti ya halmashauri hiyo kwa mwaka 2021/2022.

Diwani wa Kata ya Nyamagaro, Ezra Masana (kulia) na madiwani wengine wakishiriki kikao hicho.

Kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Ng'ong’a Gerald, ambapo madiwani mbalimbali akiwamo Ezra Masana wa Kta ya Nyamagaro wamepata nafasi ya kuchangia masuala ya uboreshaji wa huduma za jamii.

 

#MaraOnlineNews-Updates

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages