NEWS

Sunday, 20 September 2026

Simba 10 wauawa Ngorongoro, sumu yatajwa, uchunguzi waanza



Simba ndani ya NCAA

Na Mwandishi Wetu

Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA) mkoani Arusha imesema simba 10 wameuawa katika eneo la Ndutu, kata ya Endulen.

NCAA ilieleza katika taarifa yake kwa umma jana Jumamosi kwamba imebaini kuwa wanyamapori hao waliuawa Septemba 18, 2026.

“Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa wanyama hao wanaweza kuwa waliuawa kwa kulishwa sumu,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Tayari mamlaka imeanzisha uchunguzi wa kina wa kitaalamu ili kubaini chanzo na watu waliohusika katika tukio hilo.

Simba ni miongoni mwa vivutio vikubwa vya utalii vinavyotajwa kuitangaza NCAA kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages