NEWS

Thursday 23 April 2020

Daraja la zamani la Mto Mara lasombwa na maji


Daraja la zamani la Mto Mara ambalo linalouganisha Wilaya za Serengeti na Tarime limesombwa na   maji na nyumba  kadhaa kujaa maji  lakini mawasiliano  kati ya wilaya hizo hayatakatika kwa sababu tayari serikali  imeishajenga daraja jipya la kisasa kwa gharama  ya zaidi ya bilioni  nane katika eneo hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Serengeti(DC) Nurdin Babu alifika jana Alhamisi katika eneo la tukio mara tu baada ya kupata taarifa kuwa daraja hilo limesombwa na maji na kuwataka wananchi waliojirani kuhama eneo hilo mara moja baada ya nyumba zao pia kujaa maji .
Abiria wakiangalia jinsi daraja la zamani lamto Mara limesombwa na maji 

  Tumepata  habari kuwa daraja la zamani la mto Mara limesombwa na maji na kweli tumekuja na tumeshuhudia daraja halipo “, Mkuu huyo wa Wilaya alisema.
Hata hivyo wananchi walipongeza serikali kwa kujenga daraja jipya ambalo limenusuru mawasiliano kati wilaya za Tarime na Serengeti kukatika..
Viongozi wa mkoa wa Mara wakiwa katika eneo la daraja jipya  la mto Mara hivi karibuni
“ Daraja limekwenda so lisingejengwa hili mpya taarifa ingekuwa mawasiliano Tarime na Serengeti yamekatika”, alisema mwananchi mmoja kutoka eneo hilo la mto Mara.


Sehemu ya barabara ya mto Mara upande wa Tarime na Serengeyi ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami

Daraja hilo jipya limejengwa taa kubwa huku sehemu ya barabara yae upande waTarime na Serengeti ikijenwa kwa kiwano cha lami 

( Habari na Mwandishi Wetu, Mugumu)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages