NEWS

Sunday 24 May 2020

KASODEFO YAZINDUA MRADI KUKABILI CORONA



Mkurungenzi wa Kasedefo, Ezekiel Kasanga, akiongea wakati wa uzinduzi huo
TAASISI ya Kawiye Social Development Foundation (Kasodefo) yenye makao makuu wilayani Maswa, Simiyu imezindua utekelezaji wa mradi wa kukabiliana na janga la corona.



Mradi huo unalenga kuwafikia wakazi 60,000 wa wilaya hiyo iliyopo na hatimaye kuiwezesha jamii kuwa na uelewa wa kutosha dhidi ya ugonjwa huo.


Mkurugenzi wa Kasodefo, Ezekiel Kasanga, amesema hivi karibuni kwamba mradi huo umegharimu Sh milioni 30,000,000 ambazo ni ruzuku inayotolewa na shirika la Foundation for Civil Society (FCS).

Walengwa wa mradi huo ni wanawake, wazee na watoto, ambapo utekelezaji wake unahusisha viongozi wa serikali ngazi ya wilaya, idara ya afya, wenyeviti wa vijiji, viongozi wa dini, waganga wa tiba asili na wahudumu wa afya ngazi ya jamii kwa kuzingatia mpango wa taifa wa kudhibiti ugonjwa huo.                       (Imeandikwa na Anita Balingilaki, Itilima)




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages