Msaidizi wa mbunge huyo, Verediana Mgoma, ameiambia Mara Online News leo Jumapili Mei 3, 2020 kwamba tayari vijiji 86 vimeanzisha vikundi hivyo na vimeanza kugawiwa plau zinazotolewa na Profesa Muhongo.
![]() |
Wakulima wakiwa kazini Musoma vijijini |
Mgoma amesema tayari plau 45 zimeshagawiwa kwa vindundi 45 vya wakulima na kwamba mbunge huyo amejipanga kugawa nyingine 40 wakati wa Sikukuu ya Eid El Fitr baadaye mwezi huu.
![]() |
Profesa Muhongo |
Wanachama wa vikundi vya wakulima katika jimbo la Musoma Vijijini wamemshukuru mbunge wao huyo kwa hatua hizo za kuwaongezea ufanisi kwenye kilimo.
(Habari na Christopher Gamaina)
No comments:
Post a Comment