NEWS

Friday 26 June 2020

Ni shangwe tupu uzinduzi Hospitali ya Wilaya Rorya


VIONGOZI wa wilaya ya Rorya na mkoa wa Mara, leo Juni 26, 2020 wameshiriki uzinduzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya hiyo ambayo sasa iko tayari kutoa huduma za matibabu kwa wananchi.
 
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri (katikati mwenye suti nyeupe) akikata utepe kuzindua Hospitali ya Wilaya ya Rorya leo Juni 26, 2020 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima, amewakilishwa na Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri, katika uzinduzi wa hospitali hiyo.
Viongozi mbalimbali wa serikali na halmashauri wakiwemo madiwani wanaomaliza muda wao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa Hospitali ya Wilaya ya Rorya

Ujenzi wa hospitali hiyo umegharimu shilingi bilioni 1.8 zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt John Magufuli, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Charles Kitamuru Chacha.
Pichani ni viongozi  mbalimbali serikali baada ya uzinduzi wa Hospitali ya Wilaya ya Rorya
 Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Mhandisi Msafiri amesema Serikali ya Awamu ya Tano pia imeboresha huduma ya afya nchini kwa kuongeza bajeti ya dawa kutoka shilingi bilioni 33 hadi bilioni 270.

 (Habari, picha zote na Clonel Mwegendao, Rorya)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages