NEWS

Wednesday 10 July 2019

GRUMETI FUND YATOA MAFUNZO YA LUGHA YA KINGEREZA KWA WANAFUNZI 360


Na mwandishi wetu, Serengeti
Jumla ya wanafunzi 360 wa darasa la tano kutoka shule mbalimbali za msingi katika Wilaya za Serengeti na Bunda wameshirki katika kambi la kingereza ambalo huandaliwa na Grumeti Fund wakati wa likizo.
Kambi hizo zilifanyika  katika vituo vitatu  ambavyo ni kituo cha elimu ya mazingira cha Grumeti Fund, Mugumu na Bunda.
 Kila kambi lilifanyika kwa siku sita kwa lengo la kuwajengea wanafunzi hao uwezo wa kujiamini, kupenda  na kuwa na uwezo wa kujifunza kingereza.
Walimu ambao ni wabobezi  wa lugha  kutoka chuo cha Concordia kilichopo Marekani wakisadiana na walimu wa Tanzania kutoka shule husika walishiriki kutoa mafunzo hayo kwa wanafunzi hao kwa njia mbalimbali kama vile  nyimbo, kuchora, hadithi na  michezo.
Kwa kufanya hivyo wanafunzi  walengwa wataweza kumudu hata masomo mengine ambayo yanafundishwa kwa lugha ya kingereza  mara watakapojiunga na elimu ya sekondari,.
Hadi sasa wanafunzi 690 wamenufaika na mpango huo tangu mwaka 2017 ulipoanzishwa na Grumeti Fund ikiwa ni sehemu ya huduma na maendeleo  za jamii inayotoa kuchangia kuinua ubora wa sekta ya elimu katika vijiji 21 ambavyo vinapakana na mapori tengefu ya Ikorongo/Grumeti.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages