NEWS

Monday 16 September 2019

BALOZI WA TANZANIA NCHINI KENYA AMPONGEZA RAIS MAGUFULI ,KENYATTA + TAZ...



Na Mwandishi Wetu 

Balozi wa Tanzania nchini Kenya  Dkt Pindi Chana amesema mahusiano  ya Kenya na Tanzania yameendelea kuimarika kutokana uongozi bora wa  Rais John Magufuli na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta .

Dkt Chana alisema hayo juzi alipokuwa katika kilele cha maadhimisho ya nane ya siku ya Mara ambayo mwaka huu yalifanyika katika viwanja vya Sokoine Mjini  Mugumu, Wilayani Serengeti.
Mataifa ya Tanzania na Kenya  huadhimisha siku ya Mara Septemba 15 kila mwaka  kwa lengo  la kuweka mikakati ya kuhifadhi  bonde la mto Mara .

 “  Napenda kumpongeza  Mhe Rais Magufuli na  na Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta kwa kutuongoza vizuri  na sasa tunasema,Tazania na Kenya sio majirani bali ni ndugu “, Balozi Chana alisema katika mahojiano na Mara Online News .

“ Maadhimisho haya ya Mara Day  yanathibithisha kuwa sisi watanzania na wakenya tupo pamoja kujadili namna bora ya kutunza mazingira ya  bonde la mto Mara “, alisema balozi huyo wa Tanzania nchini Kenya.

Dr Chana  ambaye pia  ni mwakilishi wa kudumu wa Mpango wa Mazingira wa  Umoja wa Mataifa ( United Nations  Environment Programme) alisisitiza umuhimu wa kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages