NEWS

Friday 13 September 2019

RC AZINDUA MAADHIMISHO YA MARA DAY


Mkuu  wa Mkoa wa Mara  Adam Malima leo amezindua maadhimisho ya siku ya Mara 2019  katika viwanja vya sokoine mjini Mugumu , Wilayani Serengeti.
 RC Malima amesema  maadhimisho ya siku ya Mara ni muhmu katika uhifadhi endelevu wa  bonde la Mto Mara.
  Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Nurdin Babu  amewetaka wananchi wa Serengeti kujitokeza kwa wingi kushiriki katika maadhimisho hayo  ambayo yatahitimishwa Septemba 15.
Kaimu  Mkurugenzi wa  wa miundombinu ya uchumi na huduma za jamii  kutoka  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa   Eliabi Khalid amesema  utunzaji  wa mazingira  ya bonde la mto  Mara hauwezi kufanikiwa  bila ushirikiano mzuri baina ya Tanzania na Kenya .
Mataifa ya Tanzania na Kenya huadhimisha siku ya Mara Septemba 15 kila mwaka .
Maadimisho hayo hufanyika kwa kupokezana  ambapo mwaka  huu Tanzania ndiye itakuwa mwenyeji wa  sherehe hizo za siku ya Mara .
Kauli mbiu ya madhimsiho hayo mwaka huu ni:
“,Mimi mto Mara , Nitunze  Nikutunze”.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages