NEWS

Tuesday 15 October 2019

CHRISTIANO RONALDO AWEKA REKODI NYINGINE DUNIANI








Mshambuliaji  wa klabu ya  Juventus  na timu ya taifa ya Ureno, Christiano Ronaldo jana usiku ameweka   rekodi ya kuwa mchezaji wa tano wa muda wote duniani  kufikisha magoli 700.



Goli la 700 la Christiano Ronaldo limefungwa usiku wa kuamkia leo Jumanne Oktoba 15, 2019 dhidi ya  Ukraine kwenye mchezo wa kufuzu michuano ya  Euro.

Kwa rekodi hiyo , Ronaldo anakuwa mchezaji wa 5 kufikisha magoli 700 akiwa nyuma ya Pele mwenye magoli 757, Josef Bicangoli 756, Romario goli 749, FerencPuscas 704.

Na klabu  alizotupia magoli hayo ni Sporting Lisbon 5 , Manchester United 118,  Real Madrid 450, Juventus 32 na Ureno magoli 95

Kwa sasa Ronaldo amebakisha magoli 57 kuvunja rekodi iliyodumu muda mrefu mshambuliaji wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil,  Pele ya magoli 757








No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages