NEWS

Tuesday 14 April 2020

THAILAND YAJA NA BARAKOA ZA WATOTO WACHANGA KUWAKINGA NA COVID-19



Japokua dunia hivi leo inapambana na janga la korona maisha hayana budi kuendelea.
Hili limedhibitishwa na hospitali ya Praram 9 nchini Thailand ambapo tarehe 9  mwezi huu watoto wawili wachanga waliozaliwa walivalishwa barakoa (masks) za kutengeneza pale pale hospitali katika hatua ya kuwakinga na maambukizi ya virusi vya Corona wakiwa wanapelekwa nyumbani kutoka hospitalini walipozaliwa.
Mama wa watoto hao awali alikua ameiambia hospitali kua atatumia taxi au usafiri wa umma kwenda nao nyumbani hivyo kupelekea  manesi kuingia na hofu juu ya usalama wa watoto wale ndiposa wakabuni na kutengeneza masks kwa ajili ya kuwalinda kwa kipind hicho kifupi watokapo hospitali kuelekea nyumbani.

‘’Kinga za uso zilikua za muda mfupi’’ hospitali ilisema…kinga izo zilikua za wale watoto tu sababu ya hofu ya wao kua na hati hati ya kuambukizwa virusi hivyo kwenye usafiri  na  sio kwa ajili ya watoto wote wanaozaliwa hapa’’ walimalizia.
Pia waliongeza kua wanajali zaidi usalama.
Picha zilizopigwa kupitia kioo cha hospitali zinaonesha manesi na mama wa watoto wale wakiwa wamevaa masks wakati wamewazunguka.
Kituo cha Marekani cha kudhibhiti na kuzuia magonjwa (CDC) kinapendekeza watoto wenye miaka miwili na zaidi kuvaa masks wanapotoka kwenda kwenye hadhara ya watu ili kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona.Wataalam hao wanaamini kuwa watoto huambukizwa haraka na kusambaza bila ya wao kufahamu.

Kwa mujibu wa CDC, mtoto mchanga ni rahisi kuhusishwa na ueneaji wa virusi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine
‘’Idadi ndogo sana ya watoto wamepatikana na virusi hivyo mda mfupi tu baada ya kuzaliwa…CDC walisema kwa tafiti na taarifa za ujauzito na kunyonyesha…ingawaje haijajulikana kama watoto hao walipata kirusi hicho kabla au baada ya kuzaliwa’’.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages