NEWS

Saturday 30 May 2020

Muhongo kuchangia saruji 600 ujenzi wodi za mama, mtoto


MBUNGE wa Musoma Vijijini, Profesa Sospeter Muhongo ameanza kuchangia ujenzi wa wodi za mama na mtoto katika zahanati za vijiji vya Bukima, Nyegina na Rukuba Kisiwani.
 
Profesa Sospeter Muhongo


Profesa Muhongo ameiambia Mara Online News leo Mei 30, 2020 kwamba atachangia saruji mifuko 600, kwa mchanganuo wa mifuko 200 kwa kila zahanati, itakayotolewa kulingana na kasi ya ujenzi.

Mbunge huyo anatoa mchango huo kuunga mkono juhudi za wakazi wa vijiji hivyo na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Vijijini katika ujenzi wa wodi hizo kwa ajili ya kuboresha huduma za mama na mtoto.

(Imeandikwa na Mara Online News)


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages