NEWS

Monday 4 May 2020

Watuhumiwa mauaji ya mzee wa miaka 78 mbaroni


Kamanda Muliro Jumanne Muliro

POLISI mkoani Mwanza wamewakamata watuhumiwa wawili wa mauaji ya Ndebeto Kakula mwenye umri wa miaka 78, mkazi wa kijiji cha Mwankali wilayani Misungwi, Mwanza.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mwanza, Muliro Jumanne Muliro kwa waandishi wa habari leo Mei 4, 2020 imewataja wanaoshikiliwa kwa mauaji hayo kuwa ni Rodha Shabani (27) na Muhangwa Paul, wakazi wa kijiji cha Mwankali.

Kwa mujibu wa Kamanda Muliro, Shabani amehojiwa na kukiri kumuua mzee huyo kwa kumkata na panga shingoni wakati akitoka kuteka maji kisimani kijijini hapo, Aprili 29, 2020, saa 2:20 asubuhi.

Kamanda huyo amefafanua kuwa Shabani alitenda mauaji hayo baada ya Paul ambaye ni mganga wa kienyeji kumpigia ramli na kumwambia kwamba mzee huyo ndiye aliwaroga watoto wake wawili na kusababisha vifo vyao.

“Upelelezi wa shauri hili umekamilika kwa asilimia 90 na watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani haraka iwezekanavyo,” amesema Kamanda Muliro.


(Habari na Christopher Gamaina, Mwanza)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages