
MWILI wa askari wa Jeshi la Polisi, Garlus Mwita (36) alieuawa kwa kuchomwa mshale katika Pori Tengefu la Loliondo, wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha, umeagwa kuelekea nyumbani kwao Musoma mkoani Mara kwa ajili ya mazishi.

Akizungumza wakati wa kumuaga marehemu huyo leo Juni 12, 2022 huko Loliondo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella amewataka watu wote waliohusika katika tukio la mauaji ya askari huyo kujisalimisha kituo cha Polisi, la sivyo ajue hayuko salama.

John Mongella
Mongella amesema Serikali itawasaka watu wote watakaohujumu shughuli ya uwekaji mipaka katika Pori Tengefu la Loliondo.
#MaraOnlineNews-Updates
No comments:
Post a Comment