NEWS

Monday, 3 February 2025

Mara: Wasira ataka kero za wananchi zitatuliwe, aonya majungu CCM



Stephen Masato Wasira

Na Mwandishi Wetu, Bunda

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Masato Wasira amewakumbusha viongozi wa chama hicho tawala jukumu la kusikiliza matatizo ya wananchi na kuhakikisha yanapatiwa ufumbuzi kwa wakati.

“Lazima tusikie wananchi wanasema nini ili tuiambie serikali tuliyoiweka madarakani itatue matatizo yao,” alisema Wasira katika mkutano na viongozi, wanachama wa CCM na makundi mbalimbali ya wananchi wilayani Bunda, mkoani Mara jana Februari 2, 2025.

Alitumia nafasi hiyo pia kukemea majungu ndani ya chama hicho akitaka utendaji wa viongozi ujikite katika kutatua kero za wananchi, wakiwemo wafanyabiashara, wakulima, wavuvi na wafanyakazi.

“Vikao vyetu [CCM] vizungumze mambo ya watu. Hatuwezi kuendesha nchi bila kusikiliza watu. Na vikao vyetu viache kuzungumza majungu,” Wasira alisisitiza.
Read Also Section Example

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages