
Dkt. Samia Suluhu Hassan
Na Mwandishi Wetu
Mara
----------
Mgombea wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Oktoba 9, 2025 anaanza kuhutubia mikutano ya kampeni mkoani Mara.
Taarifa kwa umma iliyotolewa na Ofisi ya CCM Mkoa wa Mara inaeleza kuwa Dkt. Samia atahutubia mikutano ya hadhara ya wananchi katika wilaya za Butiama, Bunda, Musoma na Serengeti.
Dkt. Samia, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Taifa, ataelezea mafanikio ya Serikali yake ya Awamu ya Sita chini ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020–2025, dira na mikakati mipya ya kuimarisha maendeleo ya wananchi.
No comments:
Post a Comment