Maofisa wa forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kituo cha mpakani Sirari kilichopo Tarime mkoani Mara, wamekamata shehena ya vitenge vilivyokuwa vikiingizwa nchini kwa njia za magendo/panya kutokea nchini Kenya.
Vitenge hivyo vilivyokamatwa jana Juni 22, 2020 ni mafurushi (bales) 222 yenye mita 143,524, vyenye tamani ya shilingi milioni 136.
| Mkuu wa Wilaya ya Tarime, mhandisi Mtemi Msafiri |
Kufuatia tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri, amewakumbusha wafanyabiashara kujenga utamaduni wa kusafirisha bidhaa kwa kufuata utaratibu uliowekwa na Serikali ili kuepuka hasara zisizo za lazima.#maraonlinenewsupdate
No comments:
Post a Comment