NEWS

Tuesday 23 June 2020

Walima kahawa Mara wahakikishiwa mkopo, soko

SERIKALI imewahimiza wakulima wa kahawa mkoani Mara kuchangamkia kilimo hicho kwa kuwa imewajengea mazingira mazuri ya upatikanaji wa mkopo wa fedha na soko la zao hilo.
Mkulima wa kahawa

Mkuu wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Mhandisi Mtemi Msafiri, ameyasema hayo mjini Tarime juzi, wakati akifungua mkutano wa Wakulima wa Mara Cooperative Union (WAMACU) Ltd wanaojishughulisha na kilimo cha kahawa mkoani Mara.

“Kuna kazi kubwa inafanywa na Serikali katika kufufua mazao ya kimkakati ikiwamo kahawa, na ikumbukwe kuwa kahawa ya Tanzania inaaminika kwa ubora Afrika Mashariki,” amesema Mhandisi Msafiri na kuendelea:

“Rais [Dkt John Magufu] anataka wakulima wanufaike na kilimo, ndio maana Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeanza kuwakopesha wakulima wa kahawa fedha za uendeshaji kwa riba nafuu ya asilimia tisa, lakini pia Serikali imepata wanunuzi wa uhakika wa zao hilo.”

Hata hivyo, mkiuu huyo wa wilaya amewataka wakulima hao kujenga utamaduni wa kurejesha mikopo ya fedha kwa wakati ili kuwezesha wengine kukopa kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Mapema, Mhandisi Msafiri amesomewa taarifa ya WAMACU Ltd ambayo imetaja mafanikio ya wakulima hao kuwa ni pamoja na kupata mkopo wa shilingi bilioni 1.682 kutoka TADB, kupata ofisi na kuajiri mhasimu na meneja shughuli.

(Imeandikwa na Mara Online News)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages