NEWS

Thursday 9 July 2020

Naibu Waziri Waitara ahimiza utekelezaji miradi Tarime Vijijini


Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwita Waitara, akihutubia wanafunzi wa Shule ya Msingi Kenogo ambapo amewahimiza kusoma kwa bidii
NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara amefanya ziara katika Jimbo la Tarime Vijijini na kuhimiza watendaji wa serikali kusimamia ili kuhakikisha kuwa miradi ya maendeleo ya wananchi inayotekelezwa jimboni humo na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Ilani ya CCM inakamilika kwa wakati.

Katika ziara hiyo ya jana Julai 8, 2020, Waitara amekagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya shule za msingi na sekondari katika kata za Binagi, Nyarero, Pemba, Mbogi, Ganyange, Nyakonga na Nyamwaga.
 
Naibu Waziri wa Tamisemi, Mwita Waitara (katikati mwenye suti), akikagua maendeleo ya ujenzi wa choo katika Shule ya Msingi Soroneta
Akizungumza na makundi ya wananchi wa maeneo hayo wakiwamo walimu, madiwani, wanafunzi, watendaji wa kata na viongozi wa CCM kwa nyakati katika tofauti baada ya kukagua miradi hiyo, Naibu Waziri huyo amesema mbali ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt John Pombe Magufuli kuidhinisha elimu ya msingi na sekondari bila malipo, imetoa fedha za kugharimia uboreshaji wa mazingira ya wanafunzi kujifunza na kujifunzia.

Waitara wamewataka walimu wakuu kushirikiana na wataalamu wa idara husika na watendaji wa vijiji na kata kusimamia ili pia kuhakikisha kuwa miradi hiyo inatekelezwa kwa kiwango cha ubora uliokusudiwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages