NEWS

Tuesday 20 August 2019

KIONGOZI SDA ULIMWENGUNI ALIVYOFURAHISHWA NA MAKARIBISHO TANZANIA

TAZAMA VIDEO

                


Na Mwandishi wetu,
Kiongozi Mwenza wa  Chama  Cha Wachungaji  kutoka Makao Makuu ya kanisa la  Waadventista Wasatabo(SDA) Ulimwenguni yaliyopo Washington Marekani  Pastor Anthony Kent yupo Tarime katika kanisa la Sabasaba SDA kama mgeni maalumu katika semina ya wachungaji , wazee wa kanisa na mashemasi wa kanisa  hilo kutoka jimbo Mara ambayo imeanza leo asubuhi.
Vijana wa pathfinder wakiwa katika sehemu ya mapokezi ya wageni
Mchungaji Kent amefurahishwa  na mapokezi aliyoyapata  na kueleza kuwa anajisikia yupo nyumbani  huku akilifananisha kanisa la Sabasaba Tarime kama bustani ya edeni.
Pr Anthony Kent akiwasalimia vijana wa pathfnder kwa mapokezi mazuri waliyompa, Kuhsoto ni Pr Enock Sando ambaye ni katibu wa Mara Confrence

Akifungua mkutano huo Askofu wa Jimbo Kuu la Waadventista Wasabato(SDA) Kaskazini mwa Tanzania  Dkt Godwin Lekundayo amesema kazi kubwa ya wazee  wa kanisa ni kuwatunza washiriki  na sio tu kutoa matangazo kanisani.
Dr Lekundayo amesema watu wengi wanaobatizwa katika kanisa hilo wanapotea  kwa sababu ya kukosa mahusiano mazuri waliyoyategemea kuyapata kutoka kwa viongozi wa kanisa.
ijana wa pathfinder wakimsikiliza  Pr Kent
Katibu wa chama cha wachungaji jimbo la Mara Mchungaji Joseph  Matongo amesema wajumbe wa mkutano huo ni wachungaji na wake zao, wazee wa kanisa, mashemasi na viongozi mbalimbali wa kanisa hilo kutoka ndani nan je ya nchi .
Mkutano huo  unatarajia kumalizika Alhamisi wiki ijayo.

Kwaya ya Sabasaba SDA( Bethel)

1 comment:

  1. Congratulations!Keep it up to support the community in information technology!God uplift you more in the name of Jesus!

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages