NEWS

Monday 27 April 2020

Ng’ombe 36 wafa kwa kunywa maji yenye kemikali Nyamongo


Ng’ombe 36 na kondoo mmoja wamekufa  leo April 27 asubuhi katika kijiji cha Kewanja kilichopo Nyamongo wilayani Tarime baada ya kunywa maji yanayohofiwa kuwa na kemakali za sumu inayotokana na  maji yanayosafisha mawe ya dhahabu.
“ Ng’ombe waliokufa ni 36 na kondoo mmoja. Inahisiwa wamekunywa maji yenye yenye kemikali ya simu yanayotiririka  kutoka kwenye seneti za wachimbaji wadogo”, Mwenyekiti wa Kijiji Cha Kewanja Bunini John ameiambia Mara Online News dakika chache zilizopita.
 Mwenyekiti huyo amesema Ng’ombe waliokufa ni wa familia mbili katika kitongoji cha Kemambo.
Watu wamezuiwa kuchota maji katika eneo la tukio .

" Habari na Mwandishi Wetu, Nyamongo)


2 comments:

  1. asanteni kwa habari ila jitahidini kutoa breaking news pia habari na matukio motomoto ili media yenu ikue kwa speed

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages