NEWS

Tuesday 21 April 2020

RPC TarimeRorya ataja Majeruhi ajali ya basi na Harrier


RPC TarimeRorya William Mkonda
Watu wawili wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha basi la Kisire lenye namba T 240 DST lililogongana na gari dogo lenye namba T 823 CWR aina ya Harrier, wilayani Tarime, Mara.

Kamanda wa Polisi Tarime Rorya, William Mkonda, amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kuwataja waliojeruhiwa kuwa ni dereva wa Harrier, Wanjabu Mgonja (38) na abiria, Deogratius Makwizi (48).

Kamanda Mkonda amesema ajali hiyo imetokea Aprili 20, 2020 saa 6:30 mchana katika barabara ya Tarime – Mwanza kijijini Nyanjage.

“Majeruhi wote wamefikishwa hospitali ya Mkoa wa Mara kwa matibabu,” amesema Kamanda Mkonda.    

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages