NEWS

Tuesday 26 May 2020

Naibu Waziri Waitara apongeza ubunifu Sauti ya Mara

NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mwita Waitara, amezuru katika ofisi za Gazeti la Sauti ya Mara na Blog ya Mara Online News mjini Tarime na kupongeza ubunifu wa jina hilo na kazi za kitaaluma zinazofanywa na wafanyakazi wa vyombo hivyo vya habari.



Katika hotuba yake wakati wa ziara hiyo leo asubuhi Mei 26, 2020, Naibu Waziri Waitara amesema kitendo cha kutumia jina la Mara kwenye vyombo hivyo vya habari kinamuenzi Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambaye alizaliwa katika mkoa wa Mara.

Mhariri wa Habari, Christopher Gamaina (kulia) akimwonesha Naibu Waziri Waitara (hayupo pichani) Gazeti la Sauti ya Mara

Waitara ametumia nafasi hiyo pia kumpongeza Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Kampuni ya Mara Online inayomiliki vyombo hivyo vya habari, Mugini Jacob kwa ubunifu wa kuvianzisha na kutoa ajira kwa vijana kadhaa na kwa kuzingatia usawa wa kijinsia.



Amepongeza pia kaulimbiu ya Gazeti ya Sauti ya Mara inayosema “Habari kwa Maendeleo” akisema inachochea uandishi wa habari za maendeleo ya wananchi yakiwamo yanayowezeshwa na serikali.

Add caption

Mkuu wa kitengo cha graphics Mara online Rajabu Mpella akimueleza Naibu Waziri  wa TAMISEMI kuhusu uandaaji wa gazeti la Sauti ya Mara

Aidha, ameeleza kuvutiwa na habari zinazochapishwa na Sauti ya Mara na kuwaomba waandishi wa gazeti hilo kuendelea na sera hiyo kwa kuzingatia maadili ya taaluma ya habari.

Naye Mlezi wa Gazeti la Sauti ya Mara, Simon Mseti, amemweleza Naibu Waziri huyo kwamba anaridhishwa na mwenendo wa gazeti hilo katika kuhamasisha maendeleo ya mkoa wa Mara, Kanda ya Ziwa na Tanzania kwa jumla.

Naibu Waziri Waitara akisaini kitabu cha wageni katika ofisi za Mara Online

Kwa upande wake, CEO wa Mara Online, Jacob, amemshukuru Naibu Waziri Waitara kwa ziara hiyo na kuahidi kuzingatia ushauri wake kuhusu kuelekeza nguvu kubwa pia katika kuandika habari za kuelimisha wananchi juu ya kuepuka migogoro ya ardhi na mila zilizopitwa na wakati ikiwemo ya ukeketaji.

Naibu Waziri, Mwita Waitara (wa nne waliosimama nyuma) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Sauti ya Mara

Gazeti la Sauti ya Mara lilizinduliwa Januari 13, 2020 na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhandisi Mtemi Msafiri kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima.



(Imeandikwa na Mara Online News, Tarime)


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages