NEWS

Sunday 3 May 2020

Wanahabari Kanda ya Kati wapata viongozi


KLABU ya Waandishi wa Habari Kanda ya Kati (CPC) imechagua viongozi wapya watakaoitumikia kwa kipindi cha miaka mitano.

Akitangaza matokeo hayo jana Mei 2, 2020 jijini Dodoma, Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Abubakari Famau ambaye ni Mwakilishi wa Shirika la Utangazaji Uingereza (BBC), amesema mshindi wa nafasi ya uenyekiti ni Mussa Yusufu kutoka Uhuru Media.

Yusufu amemtangaza mshindi wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti ni Mbashiru Katare kutoka Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN).

Nafasi ya Katibu Mkuu ilichukuliwa na Benchine Bango ambaye ni mwandishi huru, huku Musa Enock kutoka AFM Radio akichaguliwa kuwa Msaidizi wake.

Waliochaguliwa kuwa wajumbe wa Kamati Tendaji ya CPC ni Jasmine Shamwepu kutoka ABM Radio, Doto Kwilasa kutoka Gazeti la Jamvi la Habari na Amani Mbando kutoka Channel Ten.

(Habari na Faustine Galafoni, Dodoma)


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages