NEWS

Tuesday, 6 August 2024

Wakenya washinda medali tatu Paris 2024


 
                     Wanariadha wa Kenya

Beatrice Chebet wa Kenya alishinda medali ya dhahabu katika mashindano ya Olimpiki mbio za mita 5,000.

Amekuwa miongoni mwa wanawake mjini Paris baada ya kushinda mbio hizo ambazo zilimfanya bingwa wa mita 1500 Faith Kipyegon kupokonywa medali ya fedha kabla ya kurejeshewa.

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 24 alivuka utepe katika dakika 14 na sekunde 28.56 mbele ya Kipyegon aliyechukua nafasi ya pili.

Kipyegon awali alinyang'anywa medali yake ya fedha baada ya kudaiwa kumzuia mwanariadha wa Ethiopia Gudaf Tsegay walipogongana katika kinyanganyiro hicho cha mita 5000.

Hata hivyo, Kipyegon hatimaye alirejeshewa medali hiyo baada ya kulalamika kwa mamlaka.

Wakati huohuo bingwa wa mbio za mita 800 Mkenya Mary Moraa alishinda medali ya shaba katika fainali ya mita 800 kwa wanawake, huku Tsige Duguma wa Ethiopia akishinda fedha nyuma ya Keely Hodgkinson wa Uingereza aliyenyakuwa dhahabu katika mbio hizo.

CHANZO:BBC
Read Also Section

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages