NEWS

Tuesday, 8 October 2024

Naibu Rais wa Kenya,Rigathi Gachagua ajitetea dhidi ya hoja ya kumwondoa madarakani

              Naibu Rais wa Kenya, Rigathi Gachagua
---------------
Kuhusu hoja iliowasilishwa na Mbunge wa Kibwezi Mwinge Mutuse, bwana Gachagua amesema kwamba madai hayo hayajafikia kiwango cha kumuondoa madarakani.

Amesema kwamba hakuna hata siku moja uchunguzi umefanywa dhidi yake kwa makosa chini ya sheria hiyo ama hata kuitwa ,kuandikisha taarifa kuhusu uchunguzi wowote.

Amesema kwamba kama Mkenya mwengine yeyote yule katiba inampa haki ya kutokuwa na hatia kuhusiana na makosa ya jinai hadi kinyume chake kitakapothibitishwa katika mahakama ya sheria chini ya kiwango maalum cha ushahidi.

Bwana Gachagua aliongezea kwamba kutokana na kutokuwepo kwa uchunguzi wowote dhidi yake haamini kwamba kunaweza kuwa na sababu zozote kuamini kwamba alifanya makosa yoyote, vinginevyo hilo lingewachiwa vyombo vya upelelezi pamoja na vyombo vya uchunguzi nchini.

‘’Kwa hivyo, ni jambo lisilowezekana kama ilivyofafanuliwa katika Ibara ya 145(1)(b) ya Katiba kutegemea maoni ya Mheshimiwa Mutuse Eckomas Mwengi bila ya kuwepo mapendekezo yoyote kutoka kwa mpelelezi .

Alisema Gachagua: Madhara halisi ya kushtakiwa kwa msingi wa madai ya makosa ya jinai ambayo ushahidi wake haujajaribiwa katika mahakama ya sheria au na vyombo vinavyotoa mamlaka ya kuchunguza kama vile DCI, Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi, Shirika la Urejeshaji Mali, Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa itakuwa kuniondoa kwenye uwezekano wa kushika wadhifa wa umma kuhusiana na Kifungu cha 99(3) bila ya utaratibu wa kisheria .
Chanzo:BBC
Read Also Section Example

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages