
Ley Matampi
Na Mwandishi Wetu
Timu ya Coastal Union ya Tanga imetangaza kuachana na aliyekuwa mlinda lango wake, Ley Matampi, 35, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwa makubaliano ya pande zote mbili.
"Tumefikia makubaliano baina ya klabu yetu na golikipa wetu Ley Matampi ya kumaliza huduma za pande zote mbili, uzoefu wako umechangia kwa asilimia kubwa mafanikio yetu ya msimu uliopota", taarifa ya Coastal imeeleza.
Mlinda mlango huyo wa zamani wa TP Mazembe alijiunga na Coastal Union msimu uliopita na kucheza kwa mafanikio makubwa mpaka kuibuka golikipa bora wa msimu wa 2023/24 wa Ligi Luu ya NBC katika tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Mjumbe Baraza Kuu UVCCM Taifa Paul Mwikwabe aanza ziara Mara, akabidhi vizibao kwa bodaboda Musoma Vijijini
>>Mgodi wa North Mara wawapa wanawake msaada wa majiko 222 ya gesi
>>HABARI PICHA:Waandishi wa habari Mara kushiriki kilele cha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
>>Rais wa Syria adaiwa kuikimbia nchi, waasi wafungulia wafungwa gerezani
No comments:
Post a Comment