
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa (JKT), Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, akipanda mti wa kumbukumbu makao makuu ya JKT, jijini Dodoma.
Dodoma
------------
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa (JKT), Dkt. Rhimo Simeon Nyansaho, Jumatatu Desemba 8, 2025, alifanya ziara ya kikazi kwa kutembelea makao makuu ya JKT, chamwino jijini Dodoma.
Mara baada ya kuwasili, Waziri Nyansaho alipokewa na mwenyeji wake, Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Mabele na uongozi mzima wa jeshi hilo.
Pamoja na mambo mengine, waziri huyo alipata wasaa wa kupanda mti wa kumbukumbu na baadaye kuzungumza na maafisa, askari na watumishi wengine.


No comments:
Post a Comment