NEWS

Monday, 5 January 2026

Waziri Nyansaho achaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Barabara Mkoa wa Mara



Waziri Dkt. Rhimo Nyansaho

Na Mwandishi Wetu
Musoma
-------------

Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mara, leo Jumanne, Januari 6, 2026 kimemchagua Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyansaho, kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo.

Awali, Mwenyekiti wa kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, amewasilisha jina la Dkt. Nyansaho, na wajumbe kwa kauli moja wakaridhia.

Kikao hicho kinachofanyika mjini Musoma, kinapokea taarifa za utekelezaji wa matengenezo ya barabara kuanzia Aprili hadi Septemba, 2025.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages