NEWS

Thursday, 12 February 2026

Serikali yatangaza neema kwa watoa habari mtandaoni




Na Godfrey Marwa,Dodoma
Serikali kupitia kwa Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo,Hamis Mwinjuma ametangaza kushuka kwa gharama za uendeshaji wa vyombo vya habari vya mtandaoni ikiwa ni sehemu ya mkakati wa serikali kuwezesha mazingira mazuri ya ufanyaji kazi kwa wanahabari badala ya kuwadhibiti.

Hayo ameyasema akiwa mgeni rasmi akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji uliofanyika jijini Dodoma leo Februari 12,2026,kwa lengo la kujadili changamoto zinazowakabili waandishi pamoja tasnia ya habari pamoja kupata taarifa ya utekelezaji wa maswala mbalimbali ya Mkutano Mkuu uliopita mwaka jana ikiwemo gharama kubwa za leseni
" Tulitoa maelekezo mahususi kwa TCRA kufanya mapitio.......,nina furaha kuwafahamisha kwamba yamefanyiwa kazi na yameleta unafuu mkubwa na wa kihistoria kwa watoa huduma mtandaoni,,amesema na kuongeza

 "Ada ya leseni imepunguzwa kwa kiasi kikubwa kutoka Shilingi laki Tano hadi elfu Hamsini,Ada ya maombi ikiwa elfu kumi pekee,vilevile kwa wakusanya maudhui mtandaoni Ada ya leseni imepunguzwa kutoka milioni moja hadi laki moja na ada ya maombi ikiwa Shilingi elfu Ishirini tu,,"ametangaza hivyo Naibu Waziri Mwinjuma.

waandishi wakishiriki mkutano jijini dodoma jana
Naibu waziri Mwinjuma ametumia fursa hiyo kuwaomba waandishi kutangaza michuano ya kandanda ya AFCON inayotarajiwa kufanyika ndani ya nchi za Afrika Mashariki mwaka 2027.
"Naomba jambo hili mlishike  muwe daraja na serikali yenu kutangaza mashindano na masula yote yanayohusu michezo kwa wananchi juu ya mi hezo hiyo itakayofanyika mwaka 2027,katika nchi tatu,Kenya Uganda na Tanzania,," 
Aidha Mamlaka ya TCR imeeleza kuwa waandishi wenye idhibati wameongezeka kutoka 300 mwaka jama hadi 3900 mwaka huu 2026,hatua ambayo wameitaja kuwa ya mafanikio makubwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages