NEWS

Saturday, 21 March 2026

Wafanyakazi wanawake Barrick North Mara wajivunia ustawi kazini



Wafanyakazi wanawake wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara wakifurahia jambo katika hafla ya Siku ya Wanawake Duniani 2026.

Na Mwandishi Wetu

Wafanyakazi wanawake wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara wamesema wanajivunia juhudi zinazofanywa na mgodi huo katika kuboresha afya, usalama na uwezeshaji wanawake kazini.

Wamesema kupitia mipango na fursa mbalimbali zinazotolewa na kampuni ya Barrick wameweza kuimarishiwa mazingira ya kazi yenye ushirikishwaji.

Wafanyakazi wanawake hao wa Barrick North Mara waliyasema hayo hivi karibuni katika taarifa yao ya mafanikio kazini kwa mwaka 2025, wakati wa hafla iliyofanyika mgodini hapo kusheherekea Siku ya Wanawake Duniani, mwaka huu.

Wafanyakazi wa Barrick North Mara wakipiga makofi katika hafla hiyo

Taarifa ilisema wafanyakazi wanawake wa mgodi huo walipata mafanikio makubwa katika kipindi cha mwaka 2025.

“Tunathamini mchango endelevu wa uongozi katika kuboresha ustawi wa wafanyakazi na kuongeza fursa kwa wanawake ndani ya kampuni,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo ilisomwa mbele ya Meneja Mkuu wa (GM) Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara, Apolinary Lyambiko.
GM Lyambiko akikabidhi cheti kwa mmoja wa wanawake hao wakati wa hafla hiyo

Wanawake hao walisema pia wamepata mafunzo ya afya ya uzazi ambayo yalijumuisha wafanyakazi wanawake na wakandarasi wa Barrick North Mara.

Kwenye medani ya kimataifa, taarifa hiyo iligusia ushiriki wa wafanyakazi wanawake wa Barrick North Mara katika Mkutano wa Wanawake wa Afrika katika masuala ya Mazingira, Afya na Usalama (African Women in EHS Conference).

Mkutano huo uliwawezesha kupata uzoefu, maendeleo ya kitaaluma, kujenga uwezo wa uongozi na mahusiano mapya.

Meneja Msaidizi wa Idara ya Mahusiano wa Barrick North Mara, Nasieku Kisambu, akisisitiza jambo katika hafla hiyo.

Kwa upande mwingine, taarifa hiyo ilisema wafanyakazi wanawake na wakandarasi 48 kutoka Barrick North Mara walishiriki maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Machi 8, 2026 yaliyofanyika kimkoa katika mji wa Mugumu, wilayani Serengeti, ikiwa ni sehemu ya msisitizo wa kampuni wa kuendeleza usawa wa kijinsia wa kutaka wanawake kujuimuika na jamii.

Kuhusu Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), taarifa hiyo ilisema wafanyakazi wanawake watano walishiriki katika mpango wa ATE Female Future, ambapo walipata ujuzi wa uongozi na fursa za maendeleo ya kitaaluma ili kuinua ubora wa utendaji na uwezo wa kushika ngazi za juu za uongozi ndani ya kampuni.
Wafanyakazi wanawake wa Barrick North Mara wakicheza katika hafla hiyo


Sehemu ya wanafanyakazi wa Barrick North Mara kwenye hafla hiyo

Taarifa hiyo iliongeza kuwa mgodi huo pia umeendelea kufanya kazi nzuri kuboresha vyumba vya makazi ya wafanyakazi wanawake.

Mgodi wa Dhahabu wa North Mara unaendeshwa na kampuni ya Barrick kwa ubia na Serikali ya Tanzania kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Wafanyakazi wa Barrick North Mara wakifurahia jambo katika hafla hiyo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages