
Mgeni rasmi, CPA Lucas Magoti, akikabidhi cheti kwa mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Magoto, wakati wa mahafali ya 11 ya kidato hicho shuleni hapo jana.
Tarime
---------------
Wanafunzi wanaoelekea kuhitimu kidato cha sita katika Shule ya Sekondari Magoto iliyopo wilayani Tarime, mkoani Mara wamehimizwa kusoma kwa bidii ili waweze kufanya vizuri katika mtihani wa taifa ujao.
Ushauri huo ulitolewa na CPA Lucas Magoti kutoka Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Tawi la Mwanza, wakati akizungumza katika Mahafali ya 11 ya Kidato cha Sita yaliyofanyika shuleni hapo jana Aprili 16, 2026.
CPA Magoti akizungumza katika mahafali hayo
Kwa upande mwingine, CPA Magoti aliahidi kuipatia shule hiyo msaada wa vifaa vya michezo vyenye thamani ya shilingi milioni moja ili kukuza vipaji vya michezo na kuimarisha afya kwa wanafunzi.
Aidha, aliahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ili kusaidia kupunguza na ikiwezekana kutatua kabisa changamoto nyingine zinazoikabili shule hiyo.
CPA Magoti na mwanafuzi wakikata keki
Akizungumza kwa niaba ya wenzake 84, mmoja wa wahitimu wa kidato cha sita katika shule hiyo, Anthony Stephano, alisema wamejipanga kikamilifu na wako tayari kuonesha matokeo yatakayoiwakilisha vyema shule yao.
Mgeni rasmi, CPA Lucas Magoto, walimu, ageni waalikwa na wanafunzi wa kidato cha sita Shule ya Sekondari Magoto katika picha ya pamoja.

Mgeni rasmi, CPA Lucas Magoti (kulia mbele), wakati wa mapokezi yake alipowasili shuleni hapo. (Picha zote na Mara Online News)

No comments:
Post a Comment