NEWS

Monday, 13 April 2026

Namba Tatu sasa akataa kuitwa mstaafu



Samwel Kiboye "Namba Tatu"

Na Mwandishi Wetu
Tarime
--------------

Aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara, Samwel Kiboye maarufu kama Namba Tatu, ametangaza rasmi kukataa kuitwa mstaafu.

“Mimi naitwa Namba Tatu, nisiitwe mstaafu, tusubiri yajao mbeleni,” Namba Tatu alisema kwa msisitizo wakati akizungumza wilayani Tarime juzi katika harambee ya ujenzi wa ofisi za makao makuu ya Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) Jimbo la North Mara Field.

Namba Tatu akimuonesha kitu Waziri Nyansaho (kushoto) katika eneo la Kanisa la SDA Kibunaye ilipofanyika harambee hiyo.

Ingawa Namba Tatu hakufafanua kauli yake hiyo, wadadisi wa masuala ya siasa za Mara wameitafsiri kama ujumbe wa kimkakati wa kupima upepo wa kisiasa kabla ya uchaguzi wa ndani ya CCM unaotarajiwa kufanyika mwakani.

Wengi wanaona kauli hiyo ya Namba Tatu ina dalili ya kuamsha ari ya wafuasi wake ili hatimaye aweze kurejea katika ulingo wa siasa za ushindani ndani ya chama hicho tawala.

Namba Tatu anatajwa kuwa miongoni mwa makada wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM Mara, akiwa na historia ya uongozi iliyoanzia ngazi ya wilaya hadi mkoa.

Aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime mwaka 2012 hadi 2017, kabla ya kushika wadhifa wa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara kuanzia mwaka 2017 hadi 2022.

Kiasi cha shilingi milioni 641 zilikunywa katika harambe hiyo ambayo iliongozwa na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Rhimo Nyanshaho, alimemwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba.

Namba Tatu ni mjumbe wa Kamati Kuu ya harambee ya kuchangia ujenzi wa ofisi hizo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages