
Mchungaji Peter Msigwa enzi zake CCM
Mchungaji Peter Msigwa, mmoja wa wanasiasa maarufu Tanzania, ambaye alihama chama cha upinzani - CHADEMA na kujiunga na chama tawala - CCM miaka kadhaa iliyopita, ametangaza kurejea chama chake cha zamani.
Katika taarifa yake kwa umma, Mchungaji Msigwa amesema amefanya uamuzi huo kwa hiari yake baada ya kufanya tafakari ya kina.
Aidha, ameomba radhi Watanzania na wanachama wa CHADEMA walioumizwa, au kukatishwa tamaa na msimamo wake wa awali, akisema hakuna binadamu asiyekosea.
No comments:
Post a Comment