
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan
-----------------------------------------
Na Mwandishi Wetu
----------------------------
Serikali ya Jamburi ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, imetangaza nafasi 11,015 za ajira za walimu nchini, zikiwemo 2,851 za walimu daraja la IIIA.
Serikali ilitangaza nafasi hizo za ajira Julai 20, 2024 kupitia Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
Mikoa wanakohitajika walimu wa daraja la IIIA na idadi yao ikiwa kwenye mabano ni Njombe (62), Mtwara (153), Dodoma (85), Shinyanga (115), Songwe (101), Iringa (56), Manyara (78), Tabora (116), Singida (110), Tanga (113) na Kagera (133).
Katavi (99), Rukwa (76), Simiyu (120), Mara (173), Geita (90), Ruvuma (140), Kigoma (129), Dar es Salaam (19), Pwani (68), Arusha (116), Mwanza (134), Morogoro (129), Kilimanjaro (124), Mbeya (217) na Lindi (95).
UNAWEZA PIA KUSOMA:
- 1.Nyambari akutana na Spika wa Bunge la Tanzania jijini New Delhi
- 2. Mwenyekiti UWT CCM Mara ahamasisha wanawake wilayani Tarime kugombea uongozi, wavuna wanachama wapya
- 3.TIC watembelea kahawa ya Tarime inayotamba soko la dunia
- 4.Balozi Mbarouk amwandikia Spika barua ya kujiuzulu ubunge
- 5.Maswi, Ridhiwan wang’ara teuzi za Rais Samia, Nape na Makamba wavuliwa uwaziri, Mashinji na Afraha wahamishwa Serengeti
No comments:
Post a Comment