Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Tulia Ackson (wa tatu kushoto) na Nyambari Nyangwine (wa pili kulia) wakiwa na wenyeji wao walipokutana Jijini New Delhi, India leo.
--------------------------------------------------
----------------------------
Mfanyabiashara na mchapishaji wa vitabu, Nyambari Nyangwine amekutana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Tulia Ackson katika Jiji la New Delhi nchini India.
Nyambari na Dkt Tulia ambaye pia ni Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), wamekutana Jijini New Delhi leo Julai 24, 2024.
Nyambari ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime mkoani Mara kupitia chama tawala - CCM, yupo nchini India tangu Jumamosi iliyopita kwa ziara ya siku nane ya kibiashara.
Akizungumza na Mara Online News kwa njia ya simu baada ya kuwasili India, Nyambari alisema alikuwa na ratiba ya kutembelea viwanda vya uchapaji vitabu katika mji wa Mumbai.
Pia, viwanda vya korosho na nguo katika mji wa Gujarat, kiwanda cha karatasi katika mji wa Kolkata na Ubalozi wa Tanzania nchini India katika Jiji la New Delhi.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
- 1. Mwenge wa Uhuru kuwasili Mara kesho, kukagua miradi ya bilioni 25/-
- 2.Oparanya na wenzake ‘wala shavu’ Baraza jipya la Mawaziri la Rais Ruto
- 3.TIC watembelea kahawa ya Tarime inayotamba soko la dunia
- 4. Mkurugenzi wa Idara ya Ulinzi wa Viongozi Marekani ajiuzulu
- 5.Rais Samia ang'oa vigogo TTCL, Posta na Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote
- 6.Balozi Mbarouk amwandikia Spika barua ya kujiuzulu ubunge
- 7.Maswi, Ridhiwan wang’ara teuzi za Rais Samia, Nape na Makamba wavuliwa uwaziri, Mashinji na Afraha wahamishwa Serengeti
No comments:
Post a Comment