
Na Mwandishi Wetu, Mwanza
Watu wanane wameripotiwa kufariki dunia na wengine 39 kujeruhiwa baada ya mabasi ya abiria ya Nyehunge na Asante Rabi kugongana leo alfajiri katika eneo la Ukirigulu, Misungwi mkoani Mwanza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, DCP Wilbroad Mutafungwa amethibitisha tukio hilo na kusema chanzo cha ajali hiyo ni basi la Asante Rabi lenye namba za usajili T 458 DYD lililokuwa likitoka Mwanza kwenda Arusha kujaribu kulipita gari jingine bila kuchukua tahadhari, kitendo kilichosababisha kugongana na basi la Nyehunge lililokuwa linatokea Morogoro kwenda Mwanza.
Kamanda Mutafungwa ametoa wito wa kuwataka madereva kuwa waangalifu zaidi barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima zinazotokana na mwendokasi na uzembe.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Shirika la MYCN lawataka vijana kuwa mabalozi wa utunzaji mazingira kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi
>>DC atoa maagizo akikabidhi pikipiki za RUWASA kwa vyombo vya huduma ya maji Tarime
>>Rock City Malls yawa kivutio cha utalii jijini Mwanza
>>MAKALA:Nyambari Nyangwine awapa vijana misingi ya kujenga taifa akihutubia mahafali ya kidato cha nne Mbezi High School
No comments:
Post a Comment