
Na Mwandishi Wetu, Bunda
Watu wanne wameripotiwa kufa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya lori aina ya Fuso lililokuwa limebeba mawe kufeli breki na kuparamia jengo lenye vibanda vya biashara mjini Bunda, Mara.
Taarifa zinaeleza kuwa ajali hiyo ilitokea jana Novemba 22, 2024 saa 5:00 asubuhi katika makutano ya barabara za Nyamuswa-Ukerewe na Musoma-Mwanza.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji wa Bunda, Dkt Yusufu Wambura alithibitisha Hospitali ya Teule ya Wilaya ya Bunda kupokea miili ya watu wanne na majeruhi sita na kwamba baadaye mmoja aliwahishwa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.
Kwa mujibu wa Dkt Wambura, mmoja wa majeruhi alilazimika kukatwa mguu kutokana na majeraha makubwa, huku mwingine akifanyiwa upasuaji.
Mbali na kusababisha vifo na majeruhi, ajali hiyo pia iliharibu mali mbalimbali za wafanyabiashara.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Barrick North Mara, Biashara United Veterani zachuana mechi za kirafiki Nyamongo
>>Biteko awatajia wananchi 'viongozi wa maendeleo' akizindua kampeni za CCM Mara
>>Mfanyabiashara wa Tanzania Nyambari Nyangwine sasa kuwekeza Uganda
>>Kamati ya Rufani Tarime yarejesha wagombea 100, CHADEMA, ACT Wazalendo waipongeza
No comments:
Post a Comment