
Waziri Innocent Bashungwa akimjulia hali majeruhi katika Hospitali Teule ya Biharamulo juzi.
----------------------------------
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amewajulia hali majeruhi wa ajali ya basi iliyosababisha vifo vya watu 11 wilayani Biharamulo, Kagera.
Bashungwa alikwenda kuwajulia hali majeruhi hao katika Hospitali Teule ya Biharamulo juzi, baada ya kutembelea eneo la Bukombe katani Nyarubango ilipotokea ajali hiyo ya basi lenye namba za usajili T 857 DHW.
Basi hilo ambalo lilikuwa linatoka Kigoma kwenda Bukoba lilisimama kushusha abiria, kisha likashindwa kuondoka na kuanza kurudi nyuma ambapo liliacha njia na kupinduka.
“Nitumie nafasi hii kuombea raho za marehemu ambao tumewapoteza katika ajali ambayo imetokea hapa Biharamulo, tumepoteza ndugu zetu 11, wametangulia mbele za haki” alisema Waziri Bashungwa
Alisema wizara yake imeanza kufanyia kazi maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ya kuwa na mfumo wa leseni za udereva ili kuwapunguzia alama hadi kuwafungia madereva wanaofanya makosa ya kuhatarisha usalama barabarani.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Hospitali Teule ya Biharamulo, Dkt Gresmus Sebuyoya, watu waliokufa katika ajali hiyo ni wanawake watano, wanaume wanne na watoto wawili.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>Mara Press haitafanya kazi na online TV, blogs ambazo hazijasajiliwa TCRA – Mugini
>>WAMACU waongoza kitaifa kwa uzalishaji kahawa bora,Benki ya Maendeleo ya Kilimo yatajwa kuchangia mafanikio hayo
>>Aliyewahi kuwa RC, Naibu Waziri ampongeza Rais Samia kwa kazi nzuri, amtabiria ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu ujao
>>Vijana TIA Kampasi ya Tanga, COHAS wafanya mazoezi ya pamoja
No comments:
Post a Comment