
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, akizungumza na waandishi wa habari (hawako pichani) jijini Dodoma leo.
----------------------------------------------
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeitisha Mkutano Mkuu Maalum utakofanyika kesho Julai 26, 2025 kwa njia ya mtandao, huku ajenda kuu ikitajwa kuwa ni marekebisho madogo ya Katiba ya chama hicho tawala.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi na Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla, amesema katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dodoma leo kwamba maabdalizi ya mkutano huo yamekamilika.
Makalla amesema kumekuwepo na maneno mengi kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mkutano huo, akisisitiza kuwa Katiba ya chama hicho inawaruhusu kufanya mkutano mkuu maalum kwa njia ya mtandao pale wanapoona inafaa.
"Maandalizi yamekamilika kwa asilimia 100, wilaya zipo tayari, mikoa yote ipo tayari, Sekretarieti tunaendelea na maandalizi ili kufanikisha mkutano huu mkuu maalum ambao utatanguliwa na vikao vya Kamati Kuu na Halmshauri Kuu ya CCM," amesema.
Unaweza pia kusoma:
»TEKNOLOJIA:Wakurugenzi Mara wapokea kompyuta 142 kuimarisha mfumo wa kidijitali vituo vya huduma za afya
»MAKALA YA MAJI:Mradi wa bilioni 21/- kuboresha huduma ya maji mjini Mugumu, RC Mara amtaka mkandarasi kuukamilisha kwa wakati
»MAKALA YA SIASA:Janeth Mtiba: Kada wa CCM mwenye umri mdogo zaidi aliyetia nia ubunge jimbo la Tarime Mjini
No comments:
Post a Comment