
Walimu na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwema wakipokea msaada wa vitabu kutoka kwa mwakilishi wa Nyambari Nyangwine Foundation, Sospeter Migera Paul (kushoto) jana Februari 13, 2025.
------------------------------------
Shule za sekondari Kurumwa, Bumera, Mwema, Korotambe na Nyabirongo zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (Vijijini) zimepokea msaada wa vitabu vya kiada na ziada kutoka Nyambari Nyangwine Foundation (NNF).
Huo ni mwendelezo wa taasisi hiyo wa kusambaza msaada wa vitabu kwenye sekondari tano kila siku.

Makabidhiano ya vitabu katika
Shule ya Sekondari Korotambe.
-------------------------------------
Mwakilishi wa taasisi hiyo, Sospeter Migera Paul alikabidhi msaada huo wa vitabu kwa kwa walimu na wanafunzi wa shule hizo kwa nyakati tofauti jana Februari 13, 2025.
Walimu na wanafunzi waliishukuru Taasisi ya Nyambari Nyangwine wakisema vitabu hivyo vitakuwa chachu ya maendeleo ya kitaaluma katika shule hizo.

Makabidhiano ya vitabu katika
Shule ya Sekondari Nyabirongo.
-------------------------------------

Makabidhiano ya vitabu katika
Shule ya Sekondari Kurumwa.
------------------------------------
Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Kurumwa iliyopo kata ya Bumera, Joseph Marwa Kisiri,akitoa neno la shkrani ameutaja msaada huo kama bahati kwao na kuahidi kusoma kwa bidii
"Hii ni bahati kwetu, tunaahidi matokeo mazuri katika mitihani yetu," mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Kurumwa, Joseph Marwa Kisiri alisema.

Mwanafunzi Joseph Marwa Kisiri (katikati)
---------------------------------
Msaada wa vitabu kwa shule za sekondari unaotolewa na Taasisi ya Nyambari Nyangwine ni sehemu ya kuunga juhudi za serikali za uwekezaji na uboreshaji wa elimu nchini kwa kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata vifaa muhimu vya kujifunzia ili waweze kufikia ndoto zao za elimu.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>HABARI PICHA:Rais Samia ashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika
>>Tarime: Heche kuchinja ng’ombe 20 kujipongeza kwa ushindi CHADEMA
>>Mwanafunzi wa sekondari afa kwa kugongwa na basi la Kisire Tarime
>>TANAPA washauriwa kujipanga kuepusha ajali za wanyamapori kugongwa na magari Nyatwali
No comments:
Post a Comment