
Mwenyekiti wa CHADEMA Jimbo la Tarime Mjini,
Bashiri Abdallah Selemani "Sauti".
---------------------------------------------
Na Mwandishi Wetu/ Mara Online News
Chama cha upinzani - CHADEMA Jimbo la Tarime Mjini kimejitabiria ushindi wa zaidi ya nusu ya mitaa yote 81 katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini kote Novemba 27, mwaka huu.
“Tumeshawapata wagombea wa mitaa yote 81, tathmini yetu inaonesha tutashinda katika mitaa 50 hadi 65,” Mwenyekiti wa CHADEMA wa jimbo hilo, Bashiri Abdallah Selemani maarufu kwa jina la Sauti aliiambia Mara Online News kwa njia ya simu jana.
Wakati huo huo, kada wa chama tawala - CCM, Ally Zedi Rajabu amehamia CHADEMA baada ya kushindwa kwenye kura za maoni za kuwania uenyekiti mtaa wa Kitaji katika jimbo la Musoma Mjini akidai ‘kuchezewa rafu’.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>MAKALA:Mwenyekiti Halmashauri Tarime Vijijini ataja miradi ya bilioni 9/- za CSR Barrick North Mara
>>Man United yamtimua Kocha Ten Hag
>>Benki ya Dunia yaridhishwa na ujenzi Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Nyerere cha Kilimo na Teknolojia
>>MAKALA MAALUMU:Ajenda ya nishati safi ya kupikia na ugumu wa biashara ya mkaa mjini Bukoba
No comments:
Post a Comment