Mfanyabiashara,Mwandishi na Mchapishaji maarufu wa vitabu nchini, Nyambari
Nyangwine, akizungumza jana jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kujiandikisha kwenye daftari la makazi la wapiga kura kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwezi ujao Novemba 27.
----------------
Nyangwine, akizungumza jana jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kujiandikisha kwenye daftari la makazi la wapiga kura kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwezi ujao Novemba 27.
----------------
Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam
Nyangwine alitoa wito huo jana baada ya kujiandikisha katika mtaa wake wa Mikocheni jijini Dar es Salaam.

“Naamini ni wajibu wangu na haki yangu kuchagua kiongozi ambaye atatufaa,” Nyangwine ambaye amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Tarime kupitia chama tawala- CCM, huku akiweka mkazo kwa Watanzania wa makundi yote katika jamii wajitokeze na kushiriki katika uchaguzi huo na kuitumia fursa hiyo kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.
Alisema ni muhimu kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa sababu maendeleo katika taifa yanaanzia kwenye ngazi hizo ambako wanaishi mamilioni ya Watanzania.
Zoezi la uandikishaji wapiga kura kwenye uchaguzi huo lilianza rasmi nchini kote Oktoba 11, 2024 na litakamilika Oktoba 20.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>MAKALA:Wananchi Nyatwali: Tunaishukuru Serikali kututua mzigo wa adha za tembo
>>RC Mara awahimiza wananchi kuchangamkia nafasi za uongozi uchaguzi Serikali za mitaa
>>MAKALA MAALUMU:Tunamuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuwafikishia wananchi huduma ya maji, hakuna atakayeachwa
>>Mwanariadha wa Kenya aweka rekodi mpya mbio za Chicago Marathon
No comments:
Post a Comment