NEWS

Tuesday, 31 December 2024

Viongozi, wadau na waandishi wa habari wakubaliana kubeba ajenda ya maendeleo Mara



Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Patrick Chandi Marwa (katikati waliokaa), viongozi wengine (waliokaa) na wadau wa uhifadhi na kilimo (waliosimama) wakati wa Mkutano Mkuu wa MRPC mjini Tarime jana Desemba 30, 2024.
-------------------------------------

Na Mara Online News, Tarime

Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mara umefanyika kwa mafanikio makubwa, huku viongozi na wadau mbalimbali wakikubaliana na waandishi hao kushirikiana katika kuchochea maendeleo ya mkoa huo.

Mbali na viongozi wa chama na serikali, wadau waliohudhuria mkutano huo ulioangazia uandishi bora kwa maendeleo ya jamii na uhifadhi endelevu, ni kutoka sekta za uhifadhi, madini na kilimo.

Wadau hao ni kutoka Hifadhi ya Taifa Serengeti (SENAPA), Grumeti Reserves, Grumeti Fund, Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara na Chama Kikuu cha Ushirika cha Wakulima wa Mara (WAMACU Ltd).


Lengo kuu la mkutano huo uliofanyika mjini Tarime jana lilikuwa kuhamasisha uandishi wa habari za maendeleo ya kijamii na kiuchumi, yakiwemo yanayochagizwa na uhifadhi wa mazingira na wanyamapori, uchimbaji madini, kilimo, ufugaji na uvuvi katika mkoa wa Mara.

Viongozi na wadau hao walieleza namna wanavyoendesha shughuli zao na kuchangia maendeleo ya jamii, kuku wakionesha kutambua umuhimu wa waandishi wa habari katika kutangaza fursa na kuhamasisha maendeleo ya kisekta.


“Waandishi wa habari ni nguzo muhimu katika maendelei ya jamii na nchi yetu, tuna kila sababu ya kuendelea kuwatumia na kuwapa support (kuwawezesha),” alisema Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Patrick Chandi Marwa aliyekuwa mgeni rasmi katika mkutano huo.
Mwenyekiti Chandi akizungumza 
katika mkutano huo.
--------------------------------

Awali, Mwenyekiti wa MRPC, Jacob Mugini alihamasisha wanachama wa klabu hiyo kuongeza nguvu ya kuandika habari zinazotangaza fursa adimu na za kipekee zilizopo mkoani Mara.

“Ni vizuri ikafahamika kwamba Mara ni mkoa wenye hifadhi bora Afrika [Hifadhi ya Taifa Serengeti], ni mkoa unaozalisha kahawa bora duniani na wenye madini mengi, lakini pia barabara ya lami nzuri,” alisema Mugini.
Mugini akizungumza katika mkutano huo.
-----------------------------------

Mkutano huo ambao ulionesha mshikamano mkubwa kati ya wanahabari, serikali na wadau wa maendeleo, ulimalizika kwa azimio la kushirikiana kuandaa kongamano la kuutangaza zaidi mkoa wa Mara.

Viongozi wengine waliohudhuria mkutano huo ni Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Meja Edward Flowin Gowele na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) CCM Wilaya, Neema Charles, miongoni mwa wengine.
Picha zote na Mara Online News
Read Also Section Example

1 comment:

  1. Ni vizuri pia kusema eneo ambalo tukio limefanyika na mawasiliano ila wapata habari pia wajue Kwa manufaa mapana ya wapata habari . Mfano eneo au ukumbi ambalo MRPC wamefanya mkutano, au habari ya KSG Kurya social group in case mtu anataka kujiunga n.k hakuna mawasiliano

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages