Zaidi ya wafungwa 1,500 wametoroka katika gereza moja nchini Msumbiji, wakitumia fursa ya machafuko ya kisiasa yanayoendelea yaliyochochewa na matokeo ya uchaguzi yenye utata, polisi wamesema.
Watu 33 waliuawa na 15 kujeruhiwa katika mapigano na walinzi, mkuu wa polisi Bernardino Rafael aliambia mkutano na waandishi wa habari.
Takriban watoro 150 zaidi wamekamatwa tena, aliongeza.
Maandamano yalizuka siku ya Jumatatu kujibu mahakama ya juu zaidi ya Msumbiji ikithibitisha kwamba chama tawala cha Frelimo, kilichokuwa madarakani tangu mwaka 1975, kilishinda uchaguzi wa rais wa Oktoba.
Bw Rafael alisema makundi ya waandamanaji wanaoipinga serikali yalikaribia gereza hilo katika mji mkuu Maputo siku ya Jumatano. Wafungwa walitumia machafuko hayo kuangusha ukuta na kutoroka, alisema.
Msumbiji imekumbwa na machafuko tangu uchaguzi uliozozaniwa mwezi Oktoba. Matokeo rasmi yalionyesha mgombea urais wa chama tawala cha Frelimo, Daniel Chapo, akishinda.
Maandamano mapya yalizuka siku ya Jumatatu, wakati mahakama ya kikatiba ilipoamua kuwa Chapo alishinda uchaguzi huo, huku ikirekebisha tofauti yake ya ushindi.
Matokeo ya awali ya mwezi Oktoba yalisema Daniel Chapo alipata asilimia 71 ya kura dhidi ya mpinzani wake mkuu Venâncio Mondlane aliyepata 20%. Mahakama sasa imeamua kwamba alishinda 65% dhidi ya 24% ya Mondlane.
Chanzo:BBC
Watu 33 waliuawa na 15 kujeruhiwa katika mapigano na walinzi, mkuu wa polisi Bernardino Rafael aliambia mkutano na waandishi wa habari.
Takriban watoro 150 zaidi wamekamatwa tena, aliongeza.
Maandamano yalizuka siku ya Jumatatu kujibu mahakama ya juu zaidi ya Msumbiji ikithibitisha kwamba chama tawala cha Frelimo, kilichokuwa madarakani tangu mwaka 1975, kilishinda uchaguzi wa rais wa Oktoba.
Bw Rafael alisema makundi ya waandamanaji wanaoipinga serikali yalikaribia gereza hilo katika mji mkuu Maputo siku ya Jumatano. Wafungwa walitumia machafuko hayo kuangusha ukuta na kutoroka, alisema.
Msumbiji imekumbwa na machafuko tangu uchaguzi uliozozaniwa mwezi Oktoba. Matokeo rasmi yalionyesha mgombea urais wa chama tawala cha Frelimo, Daniel Chapo, akishinda.
Maandamano mapya yalizuka siku ya Jumatatu, wakati mahakama ya kikatiba ilipoamua kuwa Chapo alishinda uchaguzi huo, huku ikirekebisha tofauti yake ya ushindi.
Matokeo ya awali ya mwezi Oktoba yalisema Daniel Chapo alipata asilimia 71 ya kura dhidi ya mpinzani wake mkuu Venâncio Mondlane aliyepata 20%. Mahakama sasa imeamua kwamba alishinda 65% dhidi ya 24% ya Mondlane.
Chanzo:BBC
No comments:
Post a Comment