
Diwani wa Kata ya Rabour na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Gerald Ng'ong'a.
------------------------------------
Diwani wa Kata ya Rabuor wilayani Tarime, Gerald Ng’ong’a amesema ataanza kuwalipa mshahara wenyeviti wote wa vitongoji 26 vya kata hiyo.
“Nitaanza kuwalipa wenyeviti wa vitongoji wa kata ya Rabour kila mwezi,” Ng’ong’a ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya aliimbia Mara Online News kwa simu jana.
Alisema wenyeviti 26 wote wa kata hiyo wataanza kupokea mshahara wakati wowote kuanzia sasa.
Ng’ong’a ambaye ni maarufu kwa jina la GSN alisema ameamua kufanya hivyo ili kuwezesha wenyeviti hao kuwa na ari ya kushirikiana na wananchi na viongozi wengine kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika kata hiyo.
Aidha, Diwani huyo kupitia chama tawala - CCM alisema pia amegawa msaada wa vifaa vya ofisi kwa wenyeviti hao.
Rabour ni moja ya kata zinazotajwa kupiga hatua ya maendeleo ya kjamii katika wilaya ya Rorya, mkoani Mara katika miaka ya hivi karibuni.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>TAMISEMI yatangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2025
>>Serikali yashusha shilingi trilioni 1.2 kutekeleza miradi ya maendeleo Mara
>>Mgodi wa North Mara wawapa wanawake msaada wa majiko 222 ya gesi
>>Nyambari Nyangwine kuhudhuria uzinduzi wa filamu ya vivutio vya utalii nchini India kesho
No comments:
Post a Comment