
Mkuu wa wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi (katikati waliokaa) akiwa na ujumbe wa JWTZ uliotembelea mjini Musoma jana.
-----------------------------------
Ujumbe wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ukiongozwa na Mkuu wa Utumishi wa jeshi hilo, Meja Jenerali Marco Gaguti, juzi ulianza ziara ya siku mbili ya kikazi mkoani Mara.
Jana, ujumbe huo ulifanya mazungumzo na Mkuu wa wa Mkoa wa Mara, Kanali Evans Mtambi, kuhusu masuala mbalimbali ya ulinzi na usalama.
Kanali Mtambi aliuhakikishia ujumbe huo kuwa mkoa wa Mara ni shwari na shughuli zote za maendeleo zinafanyika kawaida huku wananchi wakifurahia maisha.
Alilipongeza JWTZ kwa kazi kubwa ya ulinzi wa taifa na kutoa ushirikiano kwa mkoa wa Mara katika kuhakikisha kunakuwepo amani na usalama.
Naye Meja Jenerali Gaguti alimshukuru Kanali Mtambi kwa ushirikiano unaotolewa na mkoa wa Mara kwa shughuli za JWTZ.
UNAWEZA PIA KUSOMA:
>>CCM yakemea mbinu chafu za ‘kupita bila kupingwa’ katika uchaguzi
>>Kata za Nyarero, Nyamwaga zapata msaada wa vitabu vya sekondari kutoka Nyambari Nyangwine Foundation
>>Bunda: Taasisi ya Ryakitimbo ilivyochangia maendeleo ya wananchi Chamuriho
>>Taasisi ya Nyambari Nyangwine yazifikia kata za Manga, Kibasuka na Kiore kwa msaada wa vitabu vya sekondari
No comments:
Post a Comment